Tuesday, October 14, 2014


BURIANI BURIANI BURIANI PROFESA ALI MAZRUI

 Oktoba 14,mwaka jana Uwakilishi wa Kudumu Wa Jamhuri Y a Muungano W a Tanzania katika Umoja Wa Mataifa uliandaa hafla ya kwanza ya aina yake ya kumkumbuka na kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Hafla iliyoudhuriwa na wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi zao hapa Umoja Wa Mataifa na Wageni Mbalimbali.
Ni hafla iliyoambatana na uzinduzi wa kitabu kinachomuhusu Baba wa Taifa.Kitabu hicho kiliandikwa kwa ufundi mkubwa na Profesa Ali Mazrui kwa kushirikiana na Profesa Linda Mhando ambaye ni Mtanzania.
Uwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa umepokea kwa masikitiko makubwa  taarifa za kufariki Profesa Ali Mazrui.Ulitufunza meengi siku ile kuhusu Mwalimu na ambayo mengine hayajawahi kuandikwa popote.
Mwenyezi mungu aiweke roho ya marehemu Profesa Ali Mazrui mahala pema peponi
AMEN.

No comments:

Post a Comment