Tuesday, October 14, 2014

NEWS ALERT:LORI LA MAFUTA LAWAKA MOTO MBAGALA JIJINI DAR USIKU WA KUAMKIA LEO


Awali,lori hilo pamoja na kupiga mwereka halikufanya madhara yeyote wala dalili ya kusema litawaka moto.Ila baada ya muda likaja kundi la vijana likiwa na madumu pamoja na mifuko ya plastiki na kuanza kuchukua mafuta yalimo katika lori hilo hali iliyopelekea kutokea mlipuko mkubwa ulioteketeza kabisa lori hilo.

Haijafahamika mpaka sasa kama kuna mtu yeyote amepoteza maisha katika moto huo,ila hasara kubwa imeonekana kwa nyumba tatu zilizokuwa jirani na eneo hilo la tukio ambazo zimeteketea kabisa na moto huo.Nyumba moja ni ya makaazi ya watu,ingine ni duka la jumla la mchele pamoja na nyumba ya kulala wageni,kiwinga85.blogspot.com inaendelea kufatilia kwa ukaribu tukio hilo na tutaendelea kujuzana.
Sehemu ya lori likiwa limeteketea kabisa.
Sehemu ya wakaazi wa maeneo hayo wakiangalia kilichotokea huku wakiwa hawaamini wanachokiona.
Sehemu ya nyumba zilizoteketea kwa mtot huo.

No comments:

Post a Comment